Njia 6 rahisi za kupunguza Uzito bila Ya Kutumia diet
Kula chakula Cha usiku kabla ya saa mbili
Watu wengi huwa tunalala kuanzia saa tatu mpaka saa nne, ukila chakula baada ya saa mbili usiku inamaanisha chakula hakipati muda mzuri wa kumemenyeka kabla hujalala, wachina wengi hula chakula chao cha usiku kuanzia saa kumi na mbili na nusu jioni mpaka saa mbili usiku hii hufanya chakula chao kimemenyeke vyema kabla ya wao kwenda kulala. Hii ni tip muhimu sana kama ungependa kupungua bila ya diet.
Tafuta vyakula vya kuoka zaidi na supu supu kuliko vya kukaanga
Mafuta si mazuri mwilini, kwetu wa Tanzania bila ya kula chakula cha mafuta iwe kukaanga au rost hatuoni kama tumekula hii inasababisha mafuta kugandiana mwilini na kuongezeka mwili, kwa wenzetu wao wanachagua au upendelea kula suop na vyakula vya kuoka zaidi ambavyo huwa vina mafuta kidogo mno na viungo vichache katika kupikia.
Kutumia vyombo vidogo
Kama huwa unaangalia movie au kufuatilia vipindi vya kichina utakuwa umegundua wachina wana kawaida ya kutumia vyombo vidogo, iwe sahani, bakuli au kikombe hii ni kutaka kuto kupakua vyakula vingi kuna msemo usemao “smaller bowls = smaller portion” lakini pia kama unavyombo vikubwa basi jitahidi kujikadiria chakula cha wastani na sio kutaka kujaza chakula kutokana na ukubwa wa chombo chako.
Matunda na mboga mboga
Kula mboga mboga na matunda kunasaidia pia kufanya mwili wako upungue na uwe na afya nzuri, unaweza kula mboga mboga kama main dish na kula matunda pale unapo jisikia hamu ya kula kitu kingine baada ya kula main dish hii husaidia kutokula vitu visivyo na afya kama chocolates na biscuits.
Kwa kufanya hivyo mwili wako utapungua mpaka utaupenda.🥰🥰🥰😍😍😍
0 Comments