Advertisement

MILIKI2

FAHAMU SIFA ZA WANAUME ZINAZOWAVUTIA WANAWAKE

Mwanaume mwenye sifa hizi huwa anakuwa na mvuto zaidi katika mahusiano ya kimapenzi



 1. Sura Nzuri

Muonekano mzuri kwa mwanaume huwa ni kigezo cha kwanza katika maamuzi ya mwanzo kwa mwanamke lakini hata hivyo huwa ni katika mapenzi ya muda mfupi tu zaidi ya yale yanayodumu.

2. Ucheshi
Ucheshi kwa mwanaume si muhimu tu katika mahusiano bali humfanya mwanaume aonekane mwenye mvuto zaidi na hukumbuka mara kwa mara na mwenza wake

3. Mwanaume anayetoa msaada
Wanawake hupenda wanaume wanaotoa msaada, wasio wachoyo.... Msaada wa kifedha, nguvu(kusaidia kutokana na nguvu zako mf kusaidia kusukuma gari) na msaada wa muda(kujitoa muda wako katika jambo husika mf kuwepo pindi mwanamke ana matatizo)

4. Utajiri/Uwezo wa kifedha
Ile imani kuwa wanaume wenye uwezo wana mvuto zaidi kwa wanawake ni kweli. Utafiti ulionesha kuwa wanawake huona wanaume wanavutia zaidi pale wanaposimama tu kwenye magari ya kifahari au nyumba, hata kama vikiwa sio vyao.

5. Umri Mkubwa
Wanawake hupenda wanaume wenye umri mkubwa kwasababu mara zote huamini kuwa wamekusanya vitu vingi na uzoefu katika maisha.

6. Ndevu
Ndevu zimekuwa zikichukuliwa kama zinazokera na kuvutia kwa wakati mmoja – yote hutegemea na mapenzi ya mtu.

7. Wagumu
Wakati utafiti wa zamani unasema kuwa wanawake huvutiwa na wanaume wanawaopenda, tafiti mpya zimedai kuwa kujifanya mgumu, kutojali kunawavutia wanawake. Kifupi, wanaweza kutaka kile wanachodhani hawawezi kupata.

8. Wanawake kwenye tamaduni zote wameonesha kuvutiwa na wanaume wanaovaa rangi nyekundu

9. Wanawake wamethibitishwa pia kuwapenda wanaume majasiri na wasiogopa

Post a Comment

0 Comments