Advertisement

MILIKI2

FANYA HAYA UKUZE NYWELE ZAKO HARAKA

JE ndo umeanza safari yako ya kukuza nywele na nywele zako hazikui haraka kama ulivyotegemea? Basi inawezekana hautunzi nywele zako vizuri. Nitakuelezea njia unazoweza kutumia kukuza nywele zako haraka na kukujulisha makosa gani unayafanya yanyositisha ukuaji wa nywele zako.




MAKOSA YASABABISHAYO NYWELE ZAKO KUTOKUKUA HARAKA;
  • Kosa la kwanza, watu wengi wana blow dry au wananyoosha nywele zao mara kwa mara. Mtu akifanya hivi basi, ataziua nywele zake na zitaanza kukatika wakati wa kuchana au mda wowote. Basi inabidi upunguze kutumia vifaa kama hivi ili nywele zako zikue ( Hata kama umepaka dawa).
  • Pili, tunavyoziachia nywele kwa kuzistyle kusuka rasta, nywele za kawaida au kushonea weaving zinakubalika, ila ukizichana na kuzibana nywele basi hapo inaweza kuziharibu au kuzikata nywele.
  • Pia, kutokukata ncha baada ya mda, ncha zinaweza kuanza kuchanika na inabidi uzikate ili nywele zikue vizuri kwasababu ncha huchangia kwenye kusitisha ukuaji wa nywele na kukata nywele. Unaweza kukata ncha  cm1-2 au cm 2-2.5 baada ya miezi mitatu au minne.

MBINU ZA KUKUZA NYWELE HARAKA;

  • Kwanza, inabidi uzisuke nywele zako mara kwa mara ili zisiharibike au zisikatike. Hivi utaweza hata kuzuia ncha zilizoharibika. Kama hujisikii kusuka nywele au kushonea weaving basi unaweza kuzibana kwa juu au kuzifunga na kitambaa ila ni lazima kitambaa kiwe cha silk ili nywele zako zisiharibike  (unaweza kukitumia hata wakati wa kulala).
  • Pili, inabidi upake mafuta kwenye kichwa chako mara kwa mara, sana sana unapojisikia kama kichwa kimekauka au kama kinawasha. Mafuta mazuri kutumia kwaaji ya ukuaji wa nywele ni mafuta ya nazi, castor, Moroccan, Jamaican au lavender. Ila hata mafuta mengine yeyote ya maji unayotumia ila yasiwe ya mgando.
  • Pia, usizioshe nywele na shampu mara kwa mara kwasababu shampoo inaondoa mafuta kwenye kichwa na nywele zako. Basi, inabidi uoshe nywele na conditioner kama unaona nywele zako sio chafu sana, ila kama unaona nywele zako ni chafu basi osha na shampoo. Itakuwa bora ukipaka mafuta kabla hujaosha nywele na shampoo na uoshe nywele zako kila baada ya wiki moja na kama zinakatika basi, osha baada ya wiki mbili au tatu.
  • Kula vyakula vingi vyenye protini kama kuku, mtindi, maharagwe au nyama yyoyote
UKIZINGATIA HAYA NYWELE ZAKO ZITAKUA MPAKA UTASHANGAA💕💕💕💕

Post a Comment

0 Comments